Posts

Showing posts from December 15, 2018

WAZIRI MKUU CASSIM MAJALIWA AFUNGUA CHANELI YA UTALII

Image
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema kuwa chaneli mpya ya utalii inatarajiwa kuvutia watalii wengi zaidi kuja nchini sambamba na kuongeza pato la taifa.  Akizungumza leo jijini Dar es salaam, alipokuwa akizindua chaneli hiyo ya utalii inayojulikana kama ā€œTanzania Safari channelā€ Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa alisema kuwa chaneli hiyo mpya itatoa fursa ya kutangaza wanyama mbalimbali waliopo katika hifadhi za wanyama, utamaduni wa watanzania pamoja na vivutio mbalimbali vilivyopo nchini ili kuvutia watu wengi zaidi kuja kufanya utalii na hatimaye kuongeza kiasi cha fedha kitachochangia katika pato la taifa.  ā€œChaneli hii ni njia muhimu ya kutangaza utalii ndani na nje ya nchi yetu, ambapo itaongeza idadi ya watu watakaotembelea Tanzaniaā€ alisema Waziri Mkuu Majaliwa  Waziri Mkuu Majaliwa aliongeza kuwa kwa sasa watalii wanaokuja nchini kwa mwaka ni milioni 1.3 , na matarajio ya Serikali ni kuon...

SABABU ZA UKE KUTOA HARUFU HIZI HAPA

Image
Ni matumaini nyote mnaendelea vyema, nami alhamdulillah ala kul Hali naendelea vyema  Leo naona ni bora tukazungumzia tatizo la kutokwa na harufu mbaya ukeni maana watu wengi hudhani kuwa na harufu mbaya itokayo ukeni ni matokeo ya uchafu tu na ndio maana wanaume huwachamba wake zao kuwa hawajuhi kujisafisha na kufanya wanawake kuongeza jitihada katika kujisafisha ukeni, leo napenda kuzungumzia tatizo hili linalowasumbua wanawake wengi na kuwaumiza kichwa kutokana na kwamba lina athari kubwa sana kwani hufanya ndoa zao kudumaa NK,  -Kitaalamu Hali ya mwanamke kutokwa na maji yenye rangi nyeupe au njano ni Hali ya kawaida na sio tatizo Lakini endapo maji yanatoka yapo katika Hali ya ute mzito wenye rangi nyeupe au kahawia na yanatoa harufu kali au kuwasha hapo una tatizo  -Majimaji au ute unaoteleza kutoka sehemu za siri ni njia inayowezesha viungo vya uzazi vya mwanamke kujisafisha au kutoa uchafu wa seli zilizokufa na mabaki ya damu ya hedhi nnje ya mwili pia huviking...

SAUTI SOL WATHIBITISHA KUFANYA COLLABO NA HARMONIZE

Image
Kundi la Muziki la Sauti Sol kutoka nchini Kenya wamethibitisha kufanya kolabo la Harmonize.  Sauti Sol wamesema kuwa tayari msanii huyo alivyokuja Nairobi wakampigia wakaingia studio kwasasa kilichobaki ni kufanya video.  "Harmonize ni rafiki yetu alikuwa amekuja Nairobi akatupigia tulikua tukiambia kuwa tutafanya nyimbo all the time lakini hatukupata nafasi, this time alitupigia tulikuwa area tukampigia tuaingia studio akaua verse sasa hivi tunataka kushoot video kati ya huu mwaka au next year," Wamesema Sauti Sol walipowasili nchini

KIKOSI CHA SIMBA DHIDI YA NKANA FC LEO

Image
Kikosi cha Simba kitakachoanza dhidi ya Nkana Red Devils, Caf Champions League.  1. Aishi Manula  2. Nicolas Gyan  3. Mohamed Hussein  4. Pascal Wawa  5. Erasto Nyoni  6. James Kotei  7. Jonas Mkude  8. Clatous Chama  9. John Bocco  10. Meddie Kagere  11. Emmanuel Okwi

KAMISHNA WA TRA KUSOTA RUMANDE KWA RUSHWA

Image
Mwenyekiti wa kampuni ya Egma inayoshughulikia uwekezaji wa mitaji na dhamana, Harry Kitilya na maofisa wa zamani wa benki ya Stanbic, Shose Sinare na Sioi Solomon watamaliza mwaka wa 2018 bila ya shauri lao kuanza kusikilizwa baada ya mahakama kuambiwa jana kuwa upelelezi haujakamilika.  Kitilya, ambaye alikuwa kamishna mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Shose, ambaye alikuwa Miss Tanzania wa mwaka 1996 na Sioi, walifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa mara ya kwanza Aprili mosi 2016 na kusomewa mashtaka manane, likiwemo utakatishaji ambalo halina dhamana.  Wakili wa Serikali, Wankyo Saimon alisema jana kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika na kumuomba Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi kupanga tarehe nyingine.  Washtakiwa hao, ambao wanakabiliwa na mashtaka ya kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha fedha, wamerejeshwa rumande ambako wameshaishi kwa takribani miaka miwili sasa tangu wakamatwe.  Hakimu Shaidi alih...

HOFU YAIBUKA KAMPENI ZA UCHAGUZI YANGA

Image
Kampeni za wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi katika Klabu ya Yanga zilizopangwa kuanza juzi Alhamisi, zimeahirishwa baada ya wagombea kuhofia usalama wao.  Hiyo, ikiwa ni siku chache tangu Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imalize kuwafanyia usaili katika kuelekea uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Januari 13, mwaka huu.  Wagombea hao waliopitishwa na TFF wamekumbana na ugumu kutoka kwa wanachama wa Klabu ya Yanga ambao wanawatuhumu kuwa ni wasaliti baada ya kukubali uchaguzi wao usimamiwe na shirikisho hilo.  Jumatatu ya wiki hii katika kikao cha viongozi wa Kata Tano za Matawi ya Yanga ya jijini Dar es Salaam kilichofanyika kwenye makao makuu ya klabu hiyo Jangwani, Dar yalitolewa mapendekezo kwa wagombea hao wote kufutwa uanachama baada ya kukiuka katiba ya Klabu ya Yanga.  Kikao kiliongozwa na mwenyekiti wa Kanda ya Dar, Shabani Uda ambaye pia ni Katibu wa Tawi la Manzese ambaye alisikika akisema: ā€œHatutakwenda kupiga kura siku ya...

KIM KARDASHIAN AJIINGIZA KWENYE BIFU YA KANYE WEST NA DRAKE

Image
Baada ya sakata kati ya Kanye West na Drake kuendelea usiku wa kuamkia jana December 14,2018 kupitia ukurasa wa Twitter wa Kanye, Kim Kardashian hakutaka mumewe kupewa vitisho na hivyo kuingilia kati ugomvi huo.  Kim Kardashian ametumia page take ya twitter kumuonya Drake kuacha kumtishia maisha Mume wake kwasababu jina la Drake limetokana na Kanye West kumtengenezea njia ya yeye kujulikana, tamko hili limekuja baada ya Kanye kudai kuwa Drake amekuwa akimpigia simu na kumpa vitisho.  Baada ya Kim Kardashian kumkingia kifua mume wake alitweet ujumbe mwingine na kusema kuwa mumewe ni mwenye akili nyingi amevunja rekodi kutoboa mipaka mingi sana kila kitu kwenye muziki, ubunifu wa jukwaani, mitindo na utamaduni na ataendelea kuibadilisha dunia. 

GOLIKIPA BENO KAKOLANYA AFUKUZWA YANGA

Image
Kocha wa Yanga Mwinyi Zahera amesema hawezi tena kufanya kazi na mlinda mlango Beno Kakolanya kwasababu sio mzalendo kwa timu.  Mwinyi Zahera ameweka wazi hilo jana usiku baada ya Beno kurejea kambini kwa mara ya kwanza tangu alipotoka kwenye kambi ya timu ya taifa iliyocheza na Lesotho Novemba 18, 2018.  ''Nawaambia viongozi huyu mtu wamtafutie timu kabla ya dirisha la usajili kufungwa, simtaki tena ndani ya Yanga, timu zipo nyingi aende akacheze huko kwa waliokuwa wamemzuia kuja mazoezini'', alieleza Zahera.  Zahera amesisitiza kuwa anafahamu wakala wa mchezaji huyo ni miongoni mwa viongozi wa Simba hivyo hawezi kufanya naye kazi baada ya kupotea kwa muda mrefu sasa hana imani naye.  ''Mtu hayupo na sisi kwa muda bila sababu maalum na tulimtafuta akawa hasemi chochote sasa kwa taarifa zilizopo ni kwamba mtu anayefanya naye kazi ni kiongozi wa Simba, na kama atarudi akakaa langoni kuachia magoli itakuwaje, yeye aende tu'', aliongeza Zahera.  Yanga ip...