Posts

Showing posts from September 9, 2019

Simba kutolewa CAF ni pigo kubwa, viongozi wafunguka

Image
Meneja wa klabu ya Simba, Patrick Rweyemamu amesema kuwa klabu yake imepata hasara kwa kiasi chake baada ya kuondolewa katika hatua ya awali ya Klabu Bingwa Afrika.   Ameyasema hayo katika mazoezi ya timu hiyo yanayoendelea Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujiandaa na ratiba ya Ligi Kuu Tanzania bara (VPL).   Rweyemamu amesema kuwa hasara inaweza kuwepo au isiwepo kwa klabu hiyo kutokana na namna uwekezaji ulivyofanyika, ambapo amebainisha kuwa uwekezaji mkubwa ulikuwa katika usajili pamoja na gharama za uwekezaji.   "Gharama inaweza ikawepo au isiwepo kwa sababu msimu uliopita tulikuwa tunasafiri, posho, bonasi, visa pamoja na mahitaji mengine", amesema Rweyemamu.   "Kwa upande mwingine tumepoteza hela pia, tulikuwa tunategemea kule kama chanzo cha mapato kwa sababu tulipofika robo fainali tulipata zaidi ya  Dolla laki 6 na elfu 50 kwahiyo nao ulikuwa ni mtaji kwetu na sasa hatutoupata. Ni changamoto lakini lazima tupambane", ameongeza.   Simba ilit...

Paul Makonda akabidhi milioni 10 kwa golikipa Juma kaseja

Image
Mwenyekiti wa hamasa ya timu ya taifa (Taifastars) ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Dar es salaam  Paul makonda leo hii amemkabidhi golikipa wa taifastars Juma kasejaahadi aliyoitoa jana ya kumpa  kiasi cha shilingi milioni kumi 10 baada ya kuwa nyota wake wa mchezo wa jana uliochezwa dhidi ya burundi. Mchezo wa jana ulimalizika kwa Taifastars kufuzu hatua ya makundi baada ya kuiondoa burundi kwa mikwaju ya penati.

Habari Njema Yanga yapata mdhamini mpya amwaga mamilioni kwa wachezaji

Image
Baada Ijumaa kukusanya Sh. mil 10.8 kwenye harambee ya kuichangia Yanga iliyofanyika jijini  Dar es salaam sasa inakuja na kishindo kingine cha udhamini ambao utatikisa na kurejesha klabu hiyo kwenye hadhi yake.   Mwenyekiti wa Yanga, Dk Mshindo Msolla ameweka wazi pia kwamba kila mwezi wanatumia Sh.Mil 300 kulipa mishahara na Sh.Mil 200 kwenye gharama za uendeshaji.   Yanga wametamba kwamba ujio wa udhamini huo wa mamilioni kutoka kwenye kampuni hiyo ya nje ya Tanzania kutaisaidia klabu kukabiliana na ushindani wa Simba, wenye kiburi cha bilionea mzalendo Mohammed Dewji ā€˜MO’.   Msolla ambaye ndiye kiongozi msomi zaidi katika klabu za Ligi Kuu Bara msimu huu, licha ya kutotaja jina la kampuni hiyo lakini amesema udhamini wake utagharimu zaidi ya bilioni moja kwa mkataba wa mwaka.   ā€œNaomba nitamke wazi mbele yenu kwamba tuko njiani kupata mdhamini atakayekuwa akitoa pesa zaidi ya SportPesa kwani yeye atakuwa akitoa zaidi ya bilioni moja za Kitanzania na tay...

Cristiano Ronaldo apata dili kubwa na kampuni ya Nike

Image
Mchezaji Christiano Ronaldo ambaye ametwaa tuzo ya mwanasoka bora wa dunia mara tano, atapata dola za Kimarekani Milioni 139 katika mkataba wake na kampuni ya kutengeneza vifaa vya michezo ya Nike.   Ronaldo ambaye alijiunga na Juventus mwaka jana, akitokea Real Madrid, pia amekuwa na mkataba na kampuni kubwa ya nguo ya Marekani tangu mwaka 2004.

Mechi ya Yanga na Mbeya city yaahirishwa

Image
Bodi ya Ligi Kuu Tanzania bara imeuondoa kwenye ratiba mchezo wa ligi kuu kati ya Mbeya City na Yanga uliopangwa kuchezwa Septemba 18 mwaka huu na sasa mchezo huo utapangiwa tarahe nyingine.   Taarifa kutoka bodi ya ligi inaeleza kuwa sababu za kuondoa mchezo huo ni kuipa nafasi timu ya Yanga kujiandaa na mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Zesco ya nchini Zambia.

Ufaransa yagawa kichapo bila Mbappe na Pogba kucheza

Image
TIMU ya Taifa ya Ufaransa ikiwa bila kiungo wake mahiri, Paul Pogba na mshambuliaji Kylian Mbappe juzi ilionyesha kiwango cha juu na kufanikiwa kuichapa Albania, mabao 4-1.   Ufaransa wakiwa nyumbani kwenye mchezo huo wa kufuzu Euro ilifanikiwa kuonyesha kiwango cha juu. Kiungo Kingsley Coman, alifanikiwa kufunga mabao mawili kwenye mchezo huo, huku mengine yakifungwa na Olivier Giroud na Jonathan Ikone.   Matokeo haya yanawafanya Ufaransa kujiweka kwenye sehemu nzuri ya kufuzu kwa fainali hizo za mwaka 2020.Pogba pamoja na Mbappe walionekana wakiwa jukwaani wakitazama mchezo huo huku mara kwa mara wakijadiliana baadhi ya mambo.   Hata hivyo, mechi hiyo ilichelewa kuanza kwa dakika saba baada ya makosa kufanyika badala ya kupigwa Wimbo wa Taifa wa Albania ukapigwa wa Andorra, ambapo wachezaji wa Albania waligoma kucheza hadi wimbo wao upigwe