Posts

Showing posts from October 3, 2019

Ukweli wema sepetu kuzimia na kupoteza fahamu usiku

Image
Usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita Wema alianguka na kupoteza fahamu usiku wa manani akiwa kwenye sherehe yake ya kuzaliwa (private party) iliyofanyika nyumbani kwa dada yake, Nuru Sepetu maeneo ya Mbezi-Beach jijini Dar.   Achana na tatizo la kukondeana linalozungumzwa na wengi, Risasi linafahamu kwamba hii ni mara ya tatu kwa mwanadashosti huyo kuzimia katika siku za hivi karibuni. Kufuatia tukio hilo la Jumapili kulizuka taharuki kubwa kwa wageni mbalimbali waliofika nyumbani hapo.   Chanzo chetu makini kilisema kuwa, sherehe hiyo Wema alifanyiwa kwa kushtukizwa bila yeye kufahamu ambapo walioshiriki ni rafiki na ndugu wa karibu, jambo ambalo lilimfurahisha mno Wema na badaa ya kufurahi huku vinywaji vikiendelea ndipo lilipotokea tukio hilo la kusikitisha.   ā€œUnajua Wema alikuwa na furaha iliyopitiliza na wakati wote hakupenda kukaa wala kufanya chochote, badala yake alikuwa akipita huku na huku kuzungumza na rafiki zake ndipo alipojisikia vibaya na kudondoka kis...

KRC Genk yanusurika kipigo kutoka kwa Napolli

Image
Club ya KRC Genk baada ya kupoteza kwa magoli sita katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya RB Salzburg ya Austria wakiwa ugenini, leo walikuwa nyumbani Luminus Arena kukipiga dhidi ya Napoli ya Italia chini ya Ulinzi wa beki wao wa zamani Koulibaly.   Koulibaly alikuwa anarudi Genk timu ambayo aliwahi kuichezea miaka ya nyuma kabla ya milango kufunguka na kwenda mbele zaidi, Genk wakiwa nyumbani Napoli walitawala mchezo kwa asilimia 63 kwa asilimia 37 ndani ya dakika 25 za kwanza Napoli wakigongesha miamba mara tatu.   Hali ambayo inaonesha kuwa KRC Genk walielemewa zaidi ila game ilifanikiwa kumalizika kwa sare tasa (0-0) na Genk kuvuna point yao ya kwanza katika michuano hiyo, sasa wana kazi ya kwenda Anfield kucheza dhidi ya Liverpool kabla ya wiki mbili tena baadae kurudiana nao, Mbwana Samatta inaonekana kwa sasa ni kama nahodha msaidizi Genk kutokana na kuvaa kitambaa cha unahodha pale anapokesekana nahodha mkuu Dewaest.