Posts

Showing posts from September 11, 2019

Kim kardashian aingiza zaidi ya billioni 4 ndani ya dakika 8

Image
Utajiri wa Familia isiyoishiwa na vituko ya The Kardashian sio tu Mamilioni ya watu ambao wanawafatilia kila mahala bali ni ushawishi walionao kwa hao watu, Inaripotiwa Kuwa Kim Kardashian Siku ya Jana (Sept. 10) ameingiza zaidi ya Tsh. Billion 4.5 ( $ 2M) Ndani ya dakika chache tu baada ya bidhaa zake mpya za nguo (SKIMS) kuanza kuuzwa.   Bidhaa hizo mpya ndani ya siku moja tayari zimetajwa kuwa tishio kwa makampuni makubwa ya nguo za ndani za wanawake, Kampuni maarufu ya Spanx ilipata faida ya Dola Million 4 Mwaka wao wa Kwanza Lakini Kim K Tayari ameshaitengeneza nusu ya hizo Pesa ndani ya Dakika Tu. Hata Hivyo haishangazi sana ukiangalia na idadi ya watu wanaomfata kwenye Mitandao ya Kijamii, Kim K ana idadi ya Follower Million 147 Kwenye Instagram na Million 61.5 Kwenye Mtandao wa Twitter.   TMZ wameripoti kuwa kabla ya #KimKardashian kuziachia rasmi hizo bidhaa za nguo za wanawake alilazimika kusogeza mbele hadi siku ya Jumanne (Septemba 10) kutokana na Mtandao ulio...

Shabiki wa Yanga atembea kwa miguu hadi zambia kuangalia mpira

Image
Mwanachama na shabiki wa klabu ya Yanga leo ameanza safari ya kutembea kwa mguu kutoka Iringa kwenda Zambia kwa ajili ya mchezo wa marudiano kati ya Zesco United na Yanga mchezo ambao utachezwa September 26 katika dimba la Levvis Mwanawasa Stadium  

Mbwana samatta aendelea kuuguza majeraha ya goti

Image
Nahodha wa Taifa Stars, Mshambuliaji Mbwana Samatta, Jumapili alipata majeraha ya goti kwenye mechi dhidi ya Burundi na kumlazimu kocha kufanya mabadiliko dakika ya 106 akiingia Himid Mao.   Mara baada ya kumalizika kwa mchezo alikwea pipa (Jumatatu) na kurejea Ubelgiji katika klabu yake ya Genk.   Baada ya kufika Ubelgiji, Kupitia ukurasa wake rasmi wa mtandao wa Instagram Samatta ameeleza kuwa tayari amefanyiwa vipimo vya MRI katika goti.

Timu bora za UEFA mwaka 2019 Madrid yaongoza

Image
UEFA wametoa list ya timu bora za mpira wa miguu duniani kwa mwaka 2019. klabu ya Real madrid ikiwa imeshika  nafasi ya kwanza ikifuatiwa na Atletico Madrid nafasi ya pili na nafasi ya tatu ikishikwa na Barcelona zote za nchini uhispania. Huku upande mwingine timu za uingereza zimeongozwa na Manchester city iliyoshika nafasi ya 6 na Liverpool nafasi ya 8. Angalia picha inayofuata hapa chini kujua timu zote zilizoingia kwenye list ya uefa mwaka huu