Posts

Showing posts from September 17, 2019

Mbwana Samatta mtanzania wa kwanza kucheza na kufunga goli UEFA

Image
Ni historia mbili mpya Mbwana Samatta ameandika usiku uliopita. Amekuwa Mtanzania wa kwanza kucheza katika michuano ya Klabu bingwa Ulaya na pia wa kwanza kufunga goli kwenye michuano hiyo.   Hata hivyo, furaha yake ya kuweka rekodi binafsi imegubikwa na matokeo mabaya baada ya klabu yake ya KRC Genk kupokea kipigo kizito cha goli 6-2 kutoka kwa RB Salzburg.   Samatta alipachika bao lake wavuni katika dakika ya 52, lakini halikuweza kubadili mwelekeo wa mchezo sababu mpaka muda huo walikuwa nyuma kwa goli 5-1.   Awali kulikuwa na hofu juu ya afya ya Samatta na iwapo angecheza mechi hiyo baada ya kuumia goti alipokuwa akiitumikia timu ya Taifa ya Tanzania dhidi ya Burundi Hivi Karibuni.   Hata hivyo majeraha hayo madogo yalipona kabla ya mchezo wa jana usiku ambapo alicheza kwa dakika 85.   Mwiba mkali kwa safu ya ulinzi ya Genk alikuwa mshambuliaji Erling Braut Håland aliyepachika magoli matatu katika dakika ya dakika ya 2',34' na 45'.   Katika mchez...

Cristiano Ronaldo amlilia baba yake mzazi

Image
Ronaldo, amwaga machozi baada ya kuulizwa sawali kuhusu baba yake, Alipoulizwa jinsi alivyokuwa akijisikia baada ya  kusikia baba yake akiongea juu ya kiburi chake kwa mafanikio ya mwanawe, mchezaji huyo wa zamani wa Real Madrid aliongezea:   “Ndio.”Nadhani mahojiano yangekuwa ya kuchekesha, lakini sikutarajia kama ntalia kulia. Lakini sikuwahi kuona picha hizi wala “Sijawahi kuona video yeyote kitu ambacho hakiwezekani” Sijui iko wapi … Lazima niwe na picha hizo kuonyesha familia yangu. “Lakini sikumjua baba yangu asilimia 100. Alikuwa mtu mlevi sana. Sikuwahi kuongea naye, kama mazungumzo ya kawaida. Ilikuwa ngumu sana ”   Ronaldo aliongeza kuwa “Familia yangu imeona mafanikio yangu, mama yangu ameyaona, Ndugu zangu pia, hata mtoto wangu wa kwanza pia, lakini baba yangu, hakuona chochote, pia hakuona wakati nashinda tuzo na ilitakiwa ayaone… alikufa angali mdogo. ”