Posts

Showing posts from September 7, 2019

Billnas apinga kupewa gari na Nandy

Image
MSANII wa muziki wa Hip Hop Bongo, William Lyimo ā€˜Billnass’ ameibuka na kufungukia madai yanayosambaa mtandaoni kuwa amepewa gari na aliyekuwa mpenzi wake, Faustina Charles Mfinanga ā€˜Nandy’ kwa kusema hakuna ukweli wowote juu ya jambo hilo.    Akipinga na Risasi Jumamosi, Billnass alisema ameyaona maneno hayo mitandaoni watu wakidai kuwa Nandy amemnyang’anya gari aina ya Toyota Crown mpiga picha wake na kumpatia yeye kitu ambacho hakina ukweli, yeye anayo magari yake mawili.   ā€œUnajua watu wanapenda sana kuongea ukiangalia gari langu na la yule mpiga picha ni tofauti kabisa, watu wanaongea vitu wasivyovijua,ā€ alisema Billnass.  Aidha, Billnass alisema kuwa yeye anamiliki magari mawili ambayo yote ana kadi zake zinazosoma jina lake. ā€œMimi ninamiliki magari mawili siwezi kupewa gari na Nandy tena ambalo ameshampa mtu zawadi,ā€ alisema Billnass.   Billnass na Nandy kwa sasa wamekuwa habari ya mjini kufuatia kuachia wimbo mpya unaokwenda kwa jina la Bugana ambao ...

Zabibu kiba afunguka mume wake alivyojinusuru na Xenophobia Afrika kusini

Image
MKE wa beki wa zamani wa Simba ambaye kwa sasa anakipiga Highlands Park FC ya Afrika Kusini, Abdi Banda, Zabibu Kiba ameibuka na kuweka wazi hali ya mumewe huyo ambaye yuko Sauz ambako kuna machafuko ya Xenophobia.   Machafuko yanayoendelea nchini Afrika Kusini ya kiubaguzi yalianza Jumapili iliyopita ambapo raia wa nchini humo wamekuwa wakivamia maduka ya raia wa kigeni na kuanza kupora mali na kuchoma moto ikiwa ni pamoja na kuua watu kadhaa.   Banda amekuwa nchini Afrika Kusini kwa muda mrefu akicheza soka la kulipwa ambapo awali alikuwa akikipiga katika klabu ya Baroka kabla ya msimu huu kutua Highlands Park iliyopo Mji wa Johannesburg huku machafuko yakiwa yametokea katika Mji wa Cape Town.   Akizungumza na Championi Jumamosi, Zabibu alisema kuwa, Banda hajapatwa na matatizo ya aina yoyote kutokana na machafuko yanayoendelea nchini humo kwani yeye yupo mji mwingine.   ā€œMimi nipo huku Tanzania lakini mume wangu yupo huko Afrika Kusini na nimewasiliana naye, ...

Facebook na Instagram kuleta huduma ya mahusiano mtandaoni

Image
Facebook wameanzisha huduma mpya, maalum kwaajili ya kuanzisha mahusiano ya ukaribu zaidi baina ya watumiaji wa mtandao huo kama mapenzi na mengineyo.   Huduma hiyo tayari imeanza kupatikana katika nchi kadhaa kama Marekani, Colombia, Thailand na inatazamiwa kuanza kusambaa katika nchi nyingine hivi karibuni.   Huduma hiyo kwa sasa inapatikana katika App kuu ya Facebook hivyo mtumiaji kama unataka kujiunga, itakupasa kuunda wasifu (profile) yako nyingine na utaanza kuona marafiki kadhaa ambao wataanza kuonekana kutokana na mfanano wa taarifa mlizoweka.   Kupitia Instagram pia kipengele hicho kitaongezwa na kupewa jina la "Secret Crush", ambayo itakupa uwezo wa kuwaorodhesha marafiki zako wote kadhaa kwa siri ambao unawapenda na wao wakikubali ombi au kukuorodhesha basi mnaweza kuanzisha uhusiano wenu mnaokusudia.   Mtandao wa Facebook kwa siku za hivi karibuni umekuwa ukituhumiwa kuvujisha taarifa za watumiaji wake hivyo uanzishwaji wa huduma hiyo wachambuzi mbal...

Nandy amkataa billnas "Sio mpenzi wangu"

Image
Nandy atolea ufafanuzi juu ya ukaribu wake na Billnas ā€œMimi na Billnass hatujarudiana labda watu hawakutegemea kuona tunatoa kazi hivi karibuni, na labda video ilichangia lakini hatuna mahusiano na hata wakati tunarekodi video ya Bugana mpenzi wake alikuwepo locationā€ Nandy XXL

Sammata afunguka klabu yake kuichapa Barcelona na Madrid UEFA

Image
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amefichua kuwa alitamani kuona timu yake inapangwa na klabu ya Barcelona au Real Madrid katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.   Hivi karibuni timu ya Samatta, Genk ilipangwa kundi moja na Liverpool kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.   Samatta ambaye ni nahodha wa Taifa Stars na mshambuliaji wa KRC Genk ya Ubelgiji ametoa kauli hiyo baada ya timu yake kupangwa kwenye Kundi H, wakiwa na Liverpool, Red Bull na Napoli.   Akizungumza na Championi Ijumaa, Samatta alisema   kuwa alitamani kuona wakipangwa na timu hizo za Hispania ili kuweza kutimiza ndoto yake lakini kwa kuwa wameangukia kwa Liverpool haoni shida yoyote.   ā€œKwanza nilitamani kuona tunapangwa na Barcelona au Real Madrid hiyo ndiyo ingekuwa furaha yangu kuona naweza kucheza dhidi ya timu hizo katika michuano hiyo lakini tumeangukia kwa Liverpool siyo mbaya japo uwanja wao umekuwa mgumu.   'Lakini niseme kwamba ukiangalia kwenye ...

Rose Muhando arudi kwenye muziki wa injili na nyimbo mpya

Image
Mwimbaji Mkongwe wa nyimbo za Injili nchini, Rose Muhando ameibuka na kutoa wimbo mpya uitwao 'Walionicheka' ambao unatamba kwasasa kwenye anga za muziki wa aina hiyo.   Rose ametoa wimbo wake huo jana Alhamisi ambao amemshirikisha mwanamuziki kutoka Kenya, Ring Tone ambaye pia huimba muziki wa aina hiyo.   Kwenye wimbo huo Rose amemshukuru Mungu kwa kumvusha katika kipindi kigumu alichopitia kwani mwaka jana mwimbaji huyo akiwa nchini Kenya alipata matatizo ya kiafya ikiwemo kukumbwa na mapepo.   Rose amewahi kutamba na nyimbo kama Mteule uwe Macho, Yesu Nakupenda, Tabu Zangu, Wambea Nao, Uko Wapi na nyingine nyingi.