Posts

Showing posts from January 6, 2019

BABA AKAMATWA NA POLISI KWA KUMUUA MWANAE

Image
Hazra Mwasenga, mkazi wa Kitongoji cha Haduye Kijiji cha Iwala, Kata ya Itale wilayani Ileje, mkoani Songwe, ametiwa mbaroni kwa tuhuma za kumuua mwanawe, Subi Mwasenga (28), kwa kumkata mapanga kisha kumzika kienyeji kwa siri, akimtuhumu kuiba nyama.  Mwenyekiti wa kijiji hicho, Joseph Mwabezya, alisema tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki na aligundua alipotembelea maeneo ya makazi ya mzee huyo alimsalimia na kuuliza kuwa mwanawe haonekani na kuhoji tuta lililopo pembezoni mwa nyumba yake.  Alisema baada ya kuhoji, Mwasenga alimweleza kuwa lile tuta ni kaburi la mwanawe ambaye alimuua kwa kumkata na panga kwa kosa la kuiba nyama na kwenda kuiuza, wakati yeye alichinja ng’ombe mdogo kwa ajili ya kitoweo.  Alisema baada ya kumkata na mapanga mwanawe, alipoona amekufa aliamua kuchimba shimo na kumfukia kwa siri kwa kuwa alitenda kosa la kuiba nyama.  ā€˜ā€™Nakuomba mwenyekiti nimekueleza haya kwa kuwa wewe ni rafiki yangu, iwe siri usimwambie mtu,ā€ alisema mwenyekiti...

HUMPHREY POLEPOLE AONGEA KUHUSU BERNAD MEMBE

Image
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),Humphrey Polepole amesemaa si kweli kuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dkt. Bashiru Ally alimuitwa Bernard Membe kupitia mitandao.  Polepole ameyasema hayo kwenye mahojiano na kipindi cha Clouds 360 kupitia Clouds TV ambapo amesema kwanza ifahamike CCM ilishafunga huo mjadala na haitaki kuuongelea tena.  "Katibu Mkuu alikuwa kwenye kikao cha ndani (Hakumuita Membe mitandaoni kama inavyosemwa)," amesema Polepole.  Aliongeza kuwa 'Taarifa iliyotolewa nje ilitolewa kimakosa', amesema Polepole na kueleza kwamba CCM iliona ni busara kuachana na suala hilokwa sababu lilipotoshwa kwa kiwango kikubwa. 

WAYNE ROONEY AKAMATWA NA POLISI NCHINI MAREKANI

Image
Nahodha wa zamani wa Manchester United na timu ya Taifa ya England Wayne Rooney,  alikamatwa na Polisi katika Uwanja wa ndege wa Dulles jimbo la Virginia nchini Marekani baada ya kukutwa amekunywa dawa za usingizi pamoja na pombe ambapo ilimpelekea kuchanganyikiwa.  Mchezaji huyo alikunywa dawa hizo na pombe wakati akiwa safarini kutoka Saudi Arabia Disemba 16 mwaka jana na hivyo kupelekea kuonekana kuchanganyikiwa alipotua Uwanja wa ndege.  "Wayne Rooney alikunywa dawa za usingizi alizoagizwa kuzinywa (na daktari) akachanganya na pombe na hivyo kusababisha kuchanganyikiwa alipowasili Uwanja wa ndege ā€œ alisema msemaji wa mchezaji huyo.  Baada ya kukamatwa na polisi Rooney alitozwa dola 25 ( Tsh 50,000) na kuachiwa huru. Januari 4 alitozwa dola 91 ( Tsh 200,000) ambayo ni gharama ya kesi

TUNDU LISSU AMVAA SPIKA WA BUNGE JOB NDUGAI

Image
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antiphas Lissu amemlalamikia Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai kwa kushindwa kutimiza ahadi yake ya kwenda kumuona hospitalini kama alivyoahidi kwenye moja ya chombo cha habari nchini. Lissu ameyasema hayo kupitia Waraka huo wenye kichwa cha habari ā€˜Mwaka mpya 2019, Mwaka wa kurudisha demokrasia, haki za binadamu na utu wetu Tanzania’ Lissu amelalamika kutotembelewa na Spika wa Bunge, Job Ndugai wala watumishi wa Bunge licha ya kuahidiwa.  ā€œHadi ninapoandika maneno haya, bado Spika Ndugai hajatimiza ahadi yake hiyo. Hakuna mjumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge, au Afisa yeyote wa Bunge, aliyefika hospitalini kuniona na kunijulia hali,ā€ amesema.  Aidha kiongozi huyo amelalamika tangu kushambuliwa na watu wasiojulikana kwa risasi Septemba 7, 2017 hakuna mtu yoyote aliyehojiwa na wapelelezi  wala Jeshi la Polisi kutofanyia uchunguzi shambulio hilo.  ā€œKatika shambulio hili, hakuna anayeshukiwa na Jeshi letu la Polisi hadi sasa. Ha...

MBUNGE SUGU AMGEUKIA RAIS MAGUFULI

Image
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ā€˜Sugu’ amemtaka Rais Dkt John Pombe Magufuli kufika Jijini Mbeya kwa ajili ya kutimiza baadhi ya ahadi ambazo alizitoa wakati wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kuwa ataijenga moja ya barabara kwenye jiji hilo.  Sugu ameeleza amekuwa akitumia mikutano mbalimbali ya wananchi kumuomba Rais Magufuli kufika Jijini Mbeya ili kuzungumza na wananchi juu ya masuala mbalimbali ya shughuli za maendeleo kabla ya uchaguzi ujao.  ā€œHata mimi kwa kweli nataka sana Rais aje Mbeya na katika mikutano yangu mingi ya hadhara nimeomba Rais aje atembelee na Mbeya pia kwa sababu akichelewa sana watasema anakuja kwa vile muda wa uchaguzi umekaribia.ā€ Amesema Sugu.  ā€œNataka Rais aje kwa sababu sisi wana Mbeya zipo ahadi nyingi alizotoa wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2015, alituahidi kwamba akishinda atatusaidia maendeleo ikiwemo barabara ya Mapelele ambayo imekuwa ni kero kubwa sana kwa wananchi,ā€ aliongeza.  Awali Mbunge huyo alifika katika Shule ya...

JOSE MOURINHO AKATAA DILI LA KUFUNDISHA BENFICA

Image
Jose Mourinho akataa dili la kuifundisha klabu ya Benfica ya nchini Ureno, kocha huyo ambaye alikuwa akiifundisha klabu ya Manchester United ya Uingereza kabla ya kufutwa kazi na klabu hiyo kwa kupata matokeo mabaya katika ligi kuu ya nchi hiyo. Ikumbukwe kwasasa Mourinho hajapata timu ya kuifundisha tangia aondolewe Manchester United.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU 07/01/2019

Image