Posts

Showing posts from April, 2019

MSANII NIKKI WA PILI NA MCHUMBA WAKE WAPATA MTOTO

Image
Msanii wa muziki Bongo, Nikki wa Pili na mchumba wake wamejaliwa kupata  mtoto wa kike siku ya jana.  Rapa huyo kutoka kundi la Weusi ameeleza kuwa wamempataia mtoto wao huyo jina la Zuri. kupitia mtandao wa Twitter ameandika;  "Namshukuru Mwenyezi Mungu jana katujalia binti tumempa jina anaitwa Zuri, pili namshukuru mama zuri, safari ya kuja kwake imenifunza mengi sana,  ule mchakato wa kujifungua umefanya nizidishe mara 10000 upendo wangu na heshima yangu kwa wanawake wote duniani," ameeleza Nikki.  Utakumbuka December mwaka jana Nikki wa Pili alimvisha pete ya uchumba mpenzi wake huyo ikiwa ni wiki kadhaa tangu Bibie kuhitimu elimu yake ya Chuo Kikuu. 

EDEN HAZARD NA PAUL POGBA KUTIMKIA HISPANIA

Image
Real Madrid ya Uhispania inatarajiwa kufanya mabadiliko makubwa katika kikosi chake ifikapo mwisho wa msimu huu baada ya kuwa na msimu mbovu na kukosa makombe kama la Klabu Bingwa Ulaya na La Liga.  Pogba ambaye amekuwa akikosolewa sana siku za hivi karibuni kwa uchezaji wake anatarajiwa kuondoka Manchester United mwisho wa msimu huu kama Klabu hiyo itashindwa kupata nafasi ya kucheza Klabu Bingwa msimu ujao.  Kandarasi ya Hazard kwa Chelsea inamalizika mwisho wa msimu ujao na hadi sasa hajaonesha nia ya kutaka kusaini kandarasi nyingine, hivyo Klabu hiyo itamuacha ajiunge na Real Madrid iwapo kitita cha Paundi Milioni 100 kitalipwa.  Aidha, Hazard ni mshabiki mkubwa wa kocha wa sasa wa Madrid, Zinedine Zidane lakini pia Pogba alikaribia kujiunga Madrid miaka mitatu nyuma akitokea Juventus lakini akaishia kujiunga Man. Utd kwa ada ya Paundi Milioni 89.