LIKIZO MARUFUKU KWA WAFANYAKAZI WA UMMA - RC LINDI

Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Godfrey Zambi amepiga marufuku watumishi wa Serikali kwenda likizo kwa muda wa miezi mitatu, ili kusimamia miradi ya Maendeleo na vitambulisho vya wajasiriamali kwenye maeneo yao, na maandalizi ya mapokezi na uzimaji wa Mwenge wa Uhuru. 

Ameweka zuio hilo alipokuwa anazungumza katika kikao kazi na watumishi mbalimbali, wakiwemo Ma Ofisa Tarafa na watendaji Kata wa Halmashauri za Wilaya na Manispaa ya Lindi kilichofanyika uwanja wa Ilulu mjini humo. 

Amesema kuwa amechukua uamuzi huo kufuatia Shughuli nyingi inazoukabiri Mkoa huo kwa mwaka huu, kama vile uzimaji mwenge wa Uhuru utakaohitimisha mbio zake na kumbukizi za kifo cha hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius K. Nyerere Oktoba 14 mwaka huu na haraiki ya vijana. 

Comments