US DEMOCRATIC GOVERNOR BANNED TO ENTER AFGANISTHAN

Mbunge wa Baraza la Wawakilishi nchini Marekani, Rashida Tlaib amepewa sharti zito kutembelea Palestina baada ya waziri wa mambo ya nje wa Israel kutangaza zuio la wabunge wawili wa chama cha Democratic kufanya ziara nchini Israel pamoja na Palestina. 

Sharti hilo limetangazwa masaa machache baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani wa Israel kusema kuwa itamruhusu mbunge mmoja kuzuru Palestina kumuona bibi yake kwa sababu za kibinadamu. 

Katika ujumbe wa kijamii Ijumaa asubuhi, Tlaib aliandika hatua hiyo ingemuumiza sana kama angezuiwa hata kumuona bibi yake. 

“Uamuzi huu unatokana na kuzingatia kuwa kumtembelea bibi yangu chini ya hali hizi kandamizi ni kinyume cha kile ambacho nina imani nacho, vita dhidi ubaguzi, ukandamizaji na dhulma,” aliandika Tlaib katika barua aliyoituma kwa waziri wa mambo ya ndani wa Israeli, Aryeh Deri akiomba kuruhusiwa kumuona bibi yake 

Comments