TFF YAKATA RUFAA KUPINGA WAMBURA KURUDI KWENYE UONGOZI
Shirikisho la soka Tanzania (TFF), limekata Rufaa Mahakamani kupinga hukumu ya kumrejesha madarakani makamu wa Rais Michael Wambura ambaye amefungiwa maisha.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Desemba 14, 2018, kwenye makao makuu ya TFF, katibu mkuu wa shirikisho hilo, Wilfred Kidau amesema kesi hiyo itasimamiwa na wakili msomi Alex Mgongolwa.
Michael Wambura alichaguliwa kuwa makamu wa Rais kwenye uchaguzi wa TFF Agosti 12, 2017 jijini Dodoma.
Machi 15, 2018, Wambura alifungiwa maisha kutojihusisha na soka. Machi 25, Kamati ya Utendaji ya TFF, ilimteua Athumani Nyamlani kukaimu nafasi ya makamu wa rais wa TFF.
Novemba 30 alirudishwa kazini na mahakama ya rufaa baada ya kubaini kuwa hana makosa. Desemba 4 Wambura alikwenda TFF kupeleka barua ya mahakama lakini hakukuta kiongozi yoyote.
Baada ya kimya cha muda mrefu hatimaye leo shirikisho limeamua kuweka wazi kuwa hawawezi kufanya kazi na Wambura hivyo wamekata rufaa kupinga maamuzi ya mahakama kumrejesha madarakani
Comments
Post a Comment