HARUNA MOSHI BOBANI ASAINI MKATABA YANGA


Kiungo mshambuliaji wa klabu ya African Lyon, Haruna Moshi ‘Boban’ sasa rasmi kuwa mali ya Yanga na kinachosubiriwa ni kuanza kazi tu na wakali hao wa Jangwani.

Baada ya majadiliano ya muda mrefu, Boban kutoka African Lyon amekubaliana na Yanga kuingia mkataba wa miezi sita. 

Sasa ataanza kazi mara moja ili kuongeza nguvu katika kikosi cha Yanga ambacho kinaongoza Ligi Kuu Bara. 

Boban amewahi kuichezea Simba kwa mafanikio makubwa. Alijiunga nayo mwishoni mwaka mwaka 2003 akitokea Coastal Union ambayo baadaye alirejea tena na kuichezea.

Comments